Cristiano Ronaldo amemuomba Jose Mourinho asiiache klabu ya Real Madrid na kuelekea upande wa ligi kuu nchini Uingereza.
Kama unakumbuka mwezi uliopita kuliwahi kuwa na taarifa kwamba ‘Special One’ anampango wa kurudi nchini Uingereza kufundisha timu ya huko.
Mourinho ambaye aliondoka Chelsea mwaka 2008 na kujiunga na Inter Milan aliwahi kuhusishwa na tetesi za kushika nafasi ya kocha Sir Alex Ferguson kuifundisha Manchester United.
Lakini Ronaldo ambaye kabla ya kujiunga na Madrid alikipiga Manchetsrer United amesema kwamba Jose ni msingi wa sehemu ya mafanikio yao.
Ronaldo amesema Mourinho ni kocha mwenye mafanikio sababu ameshinda mataji kadhaa na sasa ni wakati wa kuibebesha mataji hayo klabu hiyo ya nchini Hispania.
Madrid inakabiliwa na michezo mitatu migumu dhidi ya mahasimu wao wakubwa Barcelona ikiwa ni pamoja na mchezo wa jumamosi ya tarehe 16 wa ligi ya Hispania, pia watakutana katika mchezo wa kombe la Hispania pamoja na mchezo wa nusu fainali ya klabu bingwa barani ulaya michezo yote hiyo ni ndani ya wiki mbili.
Siku ya Ijumaa Mourinho alishindwa kuuzungumzia mchezo w ao dhidi ya Barca jumamosi tarehe 16 na badala yake akimsukumia kazi hiyo kocha wake msaidizi Aitor Karanka kujibu maswali kutoka kwa waandishi wa habari.